Skip to main content

Posts

Showing posts from March 17, 2013

MWAKA MMOJA WA JIMBO

Mnamo tarehe 19/03/2012 Jimbo Katoliki la Ifakara lilizinduliwa rasmi, na Mhashamu Askofu Salutaris Libena alisimikwa rasmi kuwa Askofu wa kwanza wa Jimbo la Ifakara. Leo 19/03/2013 Jimbo la Ifakara linatimiza Mwaka Mmoja tangu kuzaliwa rasmi. Jimbo katika kuonesha shukrani kwa Mungu limeadhimisha sherehe ya Mt. Yosefu Mume wa Bikira Maria. Katika adhimisho hilo la Misa Takatifu Mhashamu Askofu Salutaris Libena alisisitiza juu ya kumshukuru Mungu kwa kutuwezesha kufanikiwa katika mambo mengi tuliyojipangia. Pia alisisitiza tuwe na Imani dhabiti kwa Mungu hasa katika Mwaka huu wa Imani. Imani hii juu ya Kristo iwe endelevu ili tuweze kufanikiwa katika mipango yetu. Misa hiyo ilihudhuriwa na Mapadre, Watawa na Walei. IFAKARA DIOCESE VIVA!