Skip to main content

Posts

Showing posts from May 12, 2013

KONGAMANO LA UTOTO MTAKATIFU WA YESU 2013

WATOTO WA UTOTO MTAKATIFU WA YESU Kongamano la Utoto Mtakatifu wa Yesu Kanda ya Mashariki 2013 litafanyika Jimboni Ifakara kuanzia tarehe 13 - 17 ya mwezi wa sita (6). Ni majimbo nane (8) yanayotarajiwa kushiriki katika Kongamano hilo. Majimbo hayo ni:- Dar es Salaam, Morogoro, Mahenge, Tanga, Zanzibar, Dodoma, Kondoa na Ifakara. Maandalizi ya Kongamano hilo yanaendelea vizuri. Mhashamu Askofu Salutaris Libena, Mapadre, Watawa na Waamini wote wa Jimbo la Ifakara wanawakaribisha Watoto wote na watu wote wenye mapenzi mema kufurahia ukarimu wa watu wa Jimbo la Ifakara..                                                     "MTOTO NA IMANI"                               KWA PAMOJA TUNASEMA KARIBUNI SANAA!!