Skip to main content

Posts

Showing posts from 2012

MBIO ZA MWAKA WA IMANI ZA PAMBAMOTO - IFAKARA

MSHUMAA MKUBWA WA MWAKA WA IMANI       Mnamo tarehe ya 17 ya mwezi wa 11 mwaka 2012, Mhashamu Askofu Salutaris M. Libena wa Jimbo Katoliki la Ifakara alizindua rasmi MWAKA WA IMANI katika Kanisa Kuu la Jimbo la Mtakatifu Andrea - Ifakara. Katika Misa hiyo Mhashamu Baba Askofu aliwasha Mshumaa Mkubwa wa Mwaka wa Imani na kisha kuwasha mishumaa midogo kutoka Mshumaa Mkubwa na kuwakabidhi Maparoko kwenda nayo Maparokiani kwo. Na ujumbe "MKAMTANGAZE KRISTO KWA KILA KIUMBE".      Miongoni mwa maazimio ya Mwaka wa Imani Jimboni Ifakara  ni kuutembeza MSALABA katika Parokia zote ndani ya Jimbo. Mbio hizo za kuutembeza Msalaba zimeanza leo tarehe 29/12/2012 kutokea Kanisa kuu la Jimbo na kwenda kukabidhiwa Parokia ya TAWETA ambayo inapakana na Jimbo la Njombe. Msalaba huo umeenda kukabidhiwa na Mhashamu Askofu Salutaris M. Libena.      Ratiba ya mzunguko  wa Msalaba huo imetoka, Safari ya Msalaba itakuwa kama ifuatavyo: Taweta, Mpanga, Mlimba, Chita, Merera, Mchombe, Mbi

TAMASHA LA SHIRIKISHO LA KWAYA ZA KIKRISTO - IFAKARA

Leo tarehe 26/12/2012 Madhehebu ya Kikristo Mjini Ifakara yamefanya Tamasha la Kwaya za Kikristo kama sehemu mojawapo ya Uinjilishaji. Maaskofu wawili walishiriki Tamasha hilo, ambao ni Mhashamu Askofu Salutaris M. Libena wa JImbo Katoliki la Ifakara na Askofu Lenard Mtenji wa KKKT Usharika wa Ifakara. Mhashamu Askofu Salutaris Libena wa Jimbo Katoliki la Ifakara aliwaambia Wanakwaya wa Kwaya zote kuwa Utume wao si kuimba kama wengine wanavyofikiri, bali UTUME WAO NI UINJILISHAJI KWA NJIA YA KUIMBA. Kwa hiyo aliwaambia wanapaswa kumshukuru Mwenyezi Mungu kwa kuwajalia sauti nzuri za kuimba, kwa hiyo wazitumie sauti hizo KUMSIFU, KUMUABUDU, KUMTUKUZA, KUMSHUKURU NA KUMTANGAZA MWENYEZI MUNGU KWA WATU WOTE. Pia aliwaomba watunzi wa nyimbo watunge nyimbo za Kumsifu, Kumtukuza na Kumshukuru Mwenyezi Mungu na Yesu Kristo zaidi kuliko kutunga nyimbo zinazomtaja SHETANI MWANZO MWISHO.Kwani tumepewa silaha za kujikinga na huyo shetani, lakini licha ya kupewa hizo kinga tumepewa sil

MWAKA WA IMANI 2012 - 2013

     Idara ya mawasiliano (J) Katoliki la Ifakara, inapenda kuwatangazia Mapadre, Watawa, Walei na watu  wenye mapenzi mema wa Jimbo la Ifakara na Kanisa kwa ujumla kuwa tarehe 17 /11 /2012 Mhashamu Baba Askofu Salutaris M. Libena atazindua rasmi MWAKA WA IMANI JIMBONI IFAKARA 2012 - 2013

THE SYNOD ON NEW EVANGELIZATION

AMECEA: Remembering the Synod on New Evangelization The Thirteen Ordinary General Assembly for the New Evangelization, which begun on 8 th October, ended on 28 th October with Holy Mass by the Holy Father, Pope Benedict XVI. The Holy Father offered a reflection on the Gospel reading of the day (John 9:39-41), which spoke about the healing of Bartimaeus, the last miracle Jesus performed before his passion.    The theme of the homily by the Holy Father was: “The New Evangelization Applies to the whole of the Church’s Life”. He stressed that the healing of Bartimaeus “represents man who needs God’s light, the light of faith, if he is to know reality truly and to walk the path of life. It is essential to acknowledge one’s blindness, one’s need for this light, otherwise one could remain blind forever. Bartimaeus represents man who has lost the light and knows it, but has not lost hope: he knows how to seize the opportunity to encounter Jesus and he entrusts himself to him for h

TANZIA

TANZIA MAREHEMU SISTA CRESENCIA NGOMBALE TAREHE 14/10/2012 Wahashamu Maaskofu wa Jimbo Katoliki la Ifakara na Mahenge, Mama Mkuu wa Shirika la Masista wa Upendo wa Mt. Fransisko wa Asizi na Jumuiya ya Mapadri na Watawa wa Majimbo yote mawili wanasikitika kwa Kifo cha Mpendwa wao Sr. Maria Cresencia B. Ngombale. Sr. M. Cresencia Benedict Ngombale ni mzaliwa wa Parokia ya Kipatimu. Alizaliwa Januari 1926 kwa wazazi, Baba:   Benedict Ngombale   Mama: Rozina Namboweto   Jina lake la ubatizo aliitwa Melania Tarehe 09/12/1945 alijiunga rasmi na Shirika la Masista wa Upendo wa Mt. Fransisko wa Asizi – Jimbo la Mahenge kwa kufunga nadhiri za kwanza. Mama Cresencia alikuwa mmojawapo kati ya kundi la pili katika shirika. Katika kipindi cha Unovisi, alisomea ualimu Kwiro – Mahenge, ambayo kwa sasa ni shule ya sekondari ya wasichana ya Mt. Agnes.   Sehemu alizokaa wakati wa uhai wake ni: Kwiro, Ifakara, Sofi, Mofu na Sali kama mwalimu wa shule ya msi

SHUKRANI YA MAVUNO

Kushukuru ni kuomba, lakini kushukuru ni Uungwana. Mhashamu Baba Askofu Salutaris Libena wa Jimbo Katoliki la Ifakara anayofuraha kubwa sana kuwaalika Mapadre,Watawa na Walei wa Jimbo la Ifakara kwenye adhimisho la Ibada ya Misa Takatifu kwa ajili ya Kumshukuru Mungu kwa Neema na Baraka mbalimbali ambazo anatujalia, katika Jimbo letu siku ya Ijumaa ya tarehe 21/09/2012 katika Kanisa Kuu la Jimbo (Ifakara).   Pia katika misa hiyo Askofu, Mapadre, Watawa na Walei wanaungana na Mapadre H. Itatiro, L. Mdenkeri na A. Magome ambao wanatimiza miaka 40 ya Upadre, pia na Padre Kawewela ambaye anatimiza miaka 25 ya Upadre.