Skip to main content

Posts

Showing posts from October 14, 2012

TANZIA

TANZIA MAREHEMU SISTA CRESENCIA NGOMBALE TAREHE 14/10/2012 Wahashamu Maaskofu wa Jimbo Katoliki la Ifakara na Mahenge, Mama Mkuu wa Shirika la Masista wa Upendo wa Mt. Fransisko wa Asizi na Jumuiya ya Mapadri na Watawa wa Majimbo yote mawili wanasikitika kwa Kifo cha Mpendwa wao Sr. Maria Cresencia B. Ngombale. Sr. M. Cresencia Benedict Ngombale ni mzaliwa wa Parokia ya Kipatimu. Alizaliwa Januari 1926 kwa wazazi, Baba:   Benedict Ngombale   Mama: Rozina Namboweto   Jina lake la ubatizo aliitwa Melania Tarehe 09/12/1945 alijiunga rasmi na Shirika la Masista wa Upendo wa Mt. Fransisko wa Asizi – Jimbo la Mahenge kwa kufunga nadhiri za kwanza. Mama Cresencia alikuwa mmojawapo kati ya kundi la pili katika shirika. Katika kipindi cha Unovisi, alisomea ualimu Kwiro – Mahenge, ambayo kwa sasa ni shule ya sekondari ya wasichana ya Mt. Agnes.   Sehemu alizokaa wakati wa uhai wake ni: Kwiro, Ifakara, Sofi, Mofu na Sali kama mwalimu wa shule ya msi