Skip to main content

KONGAMANO JIMBONI IFAKARA


KONGAMANO LA UTOTO MTAKATIFU KANDA YA MASHARIKI 13 – 17/6/2013 JIMBONI IFAKARA
 Jimbo Katoliki Ifakara lilikuwa mwenyeji wa Kongamano la mwaka huu la Utoto Mtakatifu Kanda ya
Mashariki ya Metropolitan ya Jimbo Kuu la Dar es Salaam. Kongamano hilo lilifanyika kati ya tarehe 13 na 17 Juni, 2013 lilihusisha majimbo manane ambayo ni Ifakara, Mahenge, Morogoro, Dodoma, Kondoa, Tanga, Zanzibar na Jimbo Kuu la Dar es Salaam.

Jumla ya Watoto 2 512 na walezi 570 walishiriki kongamano hili. Jumla hii ya walezi inajumuisha pia Mapadri na Watawa Masista. Maaskofu walioshiriki walikuwa ni pamoja na Mwadhama Kardinali Polycarp Pengo Askofu Mkuu wa Jimbo Kuu la Dar es Salaam, Wahashamu Maaskofu Telesphore Mkude wa Morogoro, Agapit Ndorobo wa Mahenge, Eusebius Nzigirwa Askofu Msaidizi wa Jimbo Kuu la Dar es Salaam na Askofu Mwenyeji Salutaris Libena. Jimbo mwenyeji liliwakilishwa na jumla ya watoto 875na walezi 89. Watoto na Walezi kutoka ndani ya Jimbo waliwasili Jimboni tarehe 10 Juni siku ya jumatatu kwa mazoezi ya pamoja. 

Wageni waliwasili tarehe 13 Juni siku ya jumatano. Watoto na Walezi walilala kwenye mabweni ya shule ya Benignis, sekondari ya Kilombero na Chuo cha Ufundi cha Mt. Josef. Tarehe 14 Juni, Baba Askofu Mwenyeji Salutaris Libena alilifungua rasmi kongamano kwa misa Takatifu iliyofanyika kwenye uwanja wa mpira wa kituo cha Vijana. Tarehe 15 Juni, Mhashamu Askofu Eusebius Nzigirwa aliongoza Misa Takatifu eneo hilohilo. Kwa siku mbili yaani tarehe 14 na 15 Juni, watoto na walezi wao walihudhuri semina mbalimbali zilizoongozwa na Waheshimiwa Mapadri Dr. Lucas Mahogha wa Jimbo la Mahenge, Achilleus Ndege wa Ifakara na Sr. Grace Shembetu wa Masista wa Upendo Jimbo la Mahenge. Kwa siku hizi mbili watoto walipata pia muda wa kuonyesha vipaji vyao kwa kucheza halaiki, ngoma, na michezo mingine mbalimbali.

Kilele cha Kongamanao kilikuwa tarehe 16 Juni siku ya Jumapili. Siku hiyo watoto waliamka na kupata kifungua kinywa baadaye kulifanyika Misa Takatifu kwenye uwanja wa michezo wa Kituo cha Vijana, misa iliongozwa na Mwadhama Polycarp Cardinali Pengo. Baada ya Misa Watoto na Walezi walifanya  maandamano yaliyoanzia uwanja wa Ibada hadi posta yakaelekea Soko Mjinga na kupinda kushoto eneo la Mortuary kuelekea Hospitali ya Rufaa ya Mt. Fransis hadi Kituo cha Nazareti na kumalizia kwenye uwanja wa mpira wa chuo cha Ufundi. Maandamano hayo yalipokelewa uwanjani hapo na Maaskofu wote waliohudhuria kongamano wakiongozwa na Mwadahama Kardinali Pengo.

Baada ya mlo wa mchana, saa 10 jioni watoto, walezi na Maaskofu walikusanyika tena kwenye uwanja wa mpira wa kituo cha vijana kwa kuhitimisha kongamano ambapo kila jimbo lilitoa taarifa za shughuri zake kwa kipindi cha mwaka mmoja tangu kongamano la mwaka jana ambalo lilifanyika Jimboni Dodoma. Pamoja na shughuri nyingine mbalimbali katika hitimisho hilo, Jimbo la Ifakara lilitoa zawadi rasmi kwa watoto na walezi wa Jimbo la Zanzibar. Jimbo mwenyeji lilitoa zawadi ya Msalaba na fedha taslimu shs. Laki tano. Lengo la zawadi hizo lilikuwa kuwapa pole kwa matukio ya kuvamiwa na kuuwawa na kuumizwa kwa Mapadri wao na kwa misukosuko yote wanayoipata inayohusu imani yao katoliki kutoka kwa wapinga Kristo wa huko Zanzibar. Katika hitimisho hilo, Mwenyekiti wa Maaskofu wa Kanda ya Mashariki Mwadhama Polycarp Cardinali Pengo alitangaza rasmi kuwa Kongamano la Mwaka kesho 2014 litafanyika Jimboni Kondoa. Tarehe 17 Juni wageni wote waliondoka kurudi makwao na wote walifika salama. KAULI MBIU YA KONGAMANO LA MWAKA HUU LILIKUWA MTOTO NA IMANI. Jimbo linapenda kwanza kumshukuru Mwenyeji Mungu kwa kulibariki na kuliongoza kongamano hata likafanyika na kwisha kwa usalama na amani. Pia Jimbo linapenda kuwashukuru watu wote walioshiriki kwa katika maandalizi na wakati wote wa kongamano hata likafikia malengo yake.

Comments

Popular posts from this blog

SHUKRANI YA MAVUNO

Kushukuru ni kuomba, lakini kushukuru ni Uungwana. Mhashamu Baba Askofu Salutaris Libena wa Jimbo Katoliki la Ifakara anayofuraha kubwa sana kuwaalika Mapadre,Watawa na Walei wa Jimbo la Ifakara kwenye adhimisho la Ibada ya Misa Takatifu kwa ajili ya Kumshukuru Mungu kwa Neema na Baraka mbalimbali ambazo anatujalia, katika Jimbo letu siku ya Ijumaa ya tarehe 21/09/2012 katika Kanisa Kuu la Jimbo (Ifakara).   Pia katika misa hiyo Askofu, Mapadre, Watawa na Walei wanaungana na Mapadre H. Itatiro, L. Mdenkeri na A. Magome ambao wanatimiza miaka 40 ya Upadre, pia na Padre Kawewela ambaye anatimiza miaka 25 ya Upadre. 

KONGAMANO LA UTOTO MTAKATIFU WA YESU 2013

WATOTO WA UTOTO MTAKATIFU WA YESU Kongamano la Utoto Mtakatifu wa Yesu Kanda ya Mashariki 2013 litafanyika Jimboni Ifakara kuanzia tarehe 13 - 17 ya mwezi wa sita (6). Ni majimbo nane (8) yanayotarajiwa kushiriki katika Kongamano hilo. Majimbo hayo ni:- Dar es Salaam, Morogoro, Mahenge, Tanga, Zanzibar, Dodoma, Kondoa na Ifakara. Maandalizi ya Kongamano hilo yanaendelea vizuri. Mhashamu Askofu Salutaris Libena, Mapadre, Watawa na Waamini wote wa Jimbo la Ifakara wanawakaribisha Watoto wote na watu wote wenye mapenzi mema kufurahia ukarimu wa watu wa Jimbo la Ifakara..                                                     "MTOTO NA IMANI"                               KWA PAMOJA TUNASEMA KARIBUNI SANAA!!  

PADRE LOUIS MDENKERI HATUPO NAE TENA

Padri Louis Adalbert Mdenkeri alikuwa mtoto wa tatu kati ya watoto wanane kwa baba Adalbert Fidelis Mdenkeri na mama Anthonia Kazingoma. Alizaliwa Kwiro tarehe 31 Machi, 1945. Alibatizwa tarehe 01 Aprili, 1945 namba yake ya ubatizo: Kwiro LB 15093. Alipewa kipaimara na Hayati Askofu Mkuu Edgar Maranta tarehe 01 Oktoba, 1955 namba yake ikiwa LN 10026. Alipewa daraja ya Upadri huko Kwiro tarehe 12 Agosti, 1972 na hayati Askofu Adrian Mkoba wa Morogoro.   MAREHEMU PADRE LOUIS  MDENKERI   Elimu: Hayati Padri Mdenkeli alisoma darasa la i-iv katika shule ya Msingi Kwiro. Baadaye seminari ndogo ya Mt. Fransis sasa inafahamika zaidi kama Kasita Seminari darasa la tano hadi la kumi. Baada ya kumaliza darasa la kumi pale Kasita aliacha seminari na kujiunga na sekondari ya Mt. Joseph – Jimbo Kuu la Dar es Salaam ambayo baadaye ikaja kuitwa Forodhani secondary school. Wakati anasoma St. Joseph sekondari, Hayati Sr. Yasinta aliyekuwa Mkuu wa shule alimshauri wakati huo kijana Louis Mk

HABARI ZA JIMBO -Toleo la Januari - Juni, 2015

  SIKU YA MWANAMKE DUNIANI WAWATA WAKUTANA MPANGA Tarehe 8 Machi ya kila mwaka huadhimishwa kama Siku ya Mwanamke Duniani. Kijimbo, Wanawake wakatoliki maarufu WAWATA waliiadhimisha siku ya Mwanamke Duniani ngazi ya Jimbo katika Tarafa ya Mlimba Parokiani Mpanga. Ilikuwa siku nzuri pale akina mama kutoka parokia mbalimbali walipokutana kwa semina, mafunzo mbalimbali na siku ya kilele Misa Takatifu na michezo. Mgeni rasmi katika kilele hicho alikuwa Mhe. Pd. Bonaventure Mchalange Naibu wa Askofu wa Ifakara. Mahudhurio ya akina mama kadili ya parokia yalikuwa kama inavyoonekana kwenye jedwali. Na Parokia Idadi Mwendelezo 1 Taweta 16 11 Ifakara 29 2 Mpanga 47 12 Kibaoni 10 3 Mlimba 24 13 Kiberege 2 4 Chita 12 14 Mkula 11 5 Merera 11 15 Msolwa Ujamaa 1 6 Mchombe 21 16

WATOTO WA KITUO CHA BETHLEHEM WAPATA AJALI

Watoto wapatao 103, Walezi na Wafanyakazi wa Kituo cha Bethlehem jumla yao yapata kama 160 walipata ajali ya gari siku ya jumanne ya tarehe 25 juni, 2013 majira ya saa 11 jioni wakati wakituri kutoka pikiniki. Ajali hiyo ilitokea eneo la Kijiji cha Kilama B baada ya Fuso lililo wabeba kuingia katika shimo na kuanguka. Kati ya Walezi waliopata ajali alikuwepo pia Sr. Salome. Masista wengine walezi walirudi kwa gai nyingine. Mkurugenzi wa Kituo cha Bethlehem, Padri Basil Ngwega alieleza kuwa Watoto, Walezi na Wafanyakazi wa Kituo cha Bethlehem huwa na kawaida ya kufanya pikiniki wakati wanapofunga likizo la mwaka. Na mara hii walichagua kwenda Kilama B kwa pikiniki. Aliendelea kusema kuwa wakati wakirudi, gari ambalo lilibeba kundi kubwa zaidi lilitumbukia kwenye mtaro na kuegama baadaye kuanguka upande wa kulia mwa gari. Katika ajali hiyo, watoto wapatao 20 na walezi 5 waliweza kupata majeraha mbalimbali. Kati yao watoto 2 waliumia kichwani na kushonwa na walezi 4 walipumzishwa kati

KWA HERI KATEKISTA NYONI

Parokia ya Ifakara inasikitika kumpoteza Katekista hodari Pius Pius Nyoni, ambaye Mwenyezi Mungu amependa kumuita kwake. Katekista Nyoni alizaliwa mwaka 1954 huko kijiji cha Sofi. Alipata elimu ya sekondari huko Mahenge Kwiro. Katekista  Nyoni alifanya kazi sehemu mbalimbali kabla ya kuanza kazi ya ukatekista. Alianza kazi ya Ukatekista mwaka 2003 hapa parokiani Ifakara akiwa kama mwezeshaji wa semina mbalimbali hasa katika kundi la wana uamsho. Alipelekwa chuo cha Makatekista na kisha kurudi parokiani na kuwa mwalimu wa dini mzuri. Waliofundishwa naye ndio mashaidi hasa wa utaalamu wa fani yake hii ya mwisho, yaani UALIMU WA DINI. Wote tunaalikwa kumuombea huyu ndugu yetu ambaye alifanya kazi ya Kuwafundisha watu juu ya Mungu na kuwapeleka kwa Mungu kwa mafundisho mbalimbali. APUMZIKE KWA AMANI.

TAMASHA LA SHIRIKISHO LA KWAYA ZA KIKRISTO - IFAKARA

Leo tarehe 26/12/2012 Madhehebu ya Kikristo Mjini Ifakara yamefanya Tamasha la Kwaya za Kikristo kama sehemu mojawapo ya Uinjilishaji. Maaskofu wawili walishiriki Tamasha hilo, ambao ni Mhashamu Askofu Salutaris M. Libena wa JImbo Katoliki la Ifakara na Askofu Lenard Mtenji wa KKKT Usharika wa Ifakara. Mhashamu Askofu Salutaris Libena wa Jimbo Katoliki la Ifakara aliwaambia Wanakwaya wa Kwaya zote kuwa Utume wao si kuimba kama wengine wanavyofikiri, bali UTUME WAO NI UINJILISHAJI KWA NJIA YA KUIMBA. Kwa hiyo aliwaambia wanapaswa kumshukuru Mwenyezi Mungu kwa kuwajalia sauti nzuri za kuimba, kwa hiyo wazitumie sauti hizo KUMSIFU, KUMUABUDU, KUMTUKUZA, KUMSHUKURU NA KUMTANGAZA MWENYEZI MUNGU KWA WATU WOTE. Pia aliwaomba watunzi wa nyimbo watunge nyimbo za Kumsifu, Kumtukuza na Kumshukuru Mwenyezi Mungu na Yesu Kristo zaidi kuliko kutunga nyimbo zinazomtaja SHETANI MWANZO MWISHO.Kwani tumepewa silaha za kujikinga na huyo shetani, lakini licha ya kupewa hizo kinga tumepewa sil

MBIO ZA MWAKA WA IMANI ZA PAMBAMOTO - IFAKARA

MSHUMAA MKUBWA WA MWAKA WA IMANI       Mnamo tarehe ya 17 ya mwezi wa 11 mwaka 2012, Mhashamu Askofu Salutaris M. Libena wa Jimbo Katoliki la Ifakara alizindua rasmi MWAKA WA IMANI katika Kanisa Kuu la Jimbo la Mtakatifu Andrea - Ifakara. Katika Misa hiyo Mhashamu Baba Askofu aliwasha Mshumaa Mkubwa wa Mwaka wa Imani na kisha kuwasha mishumaa midogo kutoka Mshumaa Mkubwa na kuwakabidhi Maparoko kwenda nayo Maparokiani kwo. Na ujumbe "MKAMTANGAZE KRISTO KWA KILA KIUMBE".      Miongoni mwa maazimio ya Mwaka wa Imani Jimboni Ifakara  ni kuutembeza MSALABA katika Parokia zote ndani ya Jimbo. Mbio hizo za kuutembeza Msalaba zimeanza leo tarehe 29/12/2012 kutokea Kanisa kuu la Jimbo na kwenda kukabidhiwa Parokia ya TAWETA ambayo inapakana na Jimbo la Njombe. Msalaba huo umeenda kukabidhiwa na Mhashamu Askofu Salutaris M. Libena.      Ratiba ya mzunguko  wa Msalaba huo imetoka, Safari ya Msalaba itakuwa kama ifuatavyo: Taweta, Mpanga, Mlimba, Chita, Merera, Mchombe, Mbi

MWAKA WA IMANI 2012 - 2013

     Idara ya mawasiliano (J) Katoliki la Ifakara, inapenda kuwatangazia Mapadre, Watawa, Walei na watu  wenye mapenzi mema wa Jimbo la Ifakara na Kanisa kwa ujumla kuwa tarehe 17 /11 /2012 Mhashamu Baba Askofu Salutaris M. Libena atazindua rasmi MWAKA WA IMANI JIMBONI IFAKARA 2012 - 2013