Watoto
wapatao 103, Walezi na Wafanyakazi wa Kituo cha Bethlehem jumla yao yapata kama
160 walipata ajali ya gari siku ya jumanne ya tarehe 25 juni, 2013 majira ya
saa 11 jioni wakati wakituri kutoka pikiniki. Ajali hiyo ilitokea eneo la
Kijiji cha Kilama B baada ya Fuso lililo wabeba kuingia katika shimo na kuanguka.
Kati ya Walezi waliopata ajali alikuwepo pia Sr. Salome. Masista wengine walezi
walirudi kwa gai nyingine. Mkurugenzi wa Kituo cha Bethlehem, Padri Basil Ngwega
alieleza kuwa Watoto, Walezi na Wafanyakazi wa Kituo cha Bethlehem huwa na
kawaida ya kufanya pikiniki wakati wanapofunga likizo la mwaka. Na mara hii
walichagua kwenda Kilama B kwa pikiniki. Aliendelea kusema kuwa wakati
wakirudi, gari ambalo lilibeba kundi kubwa zaidi lilitumbukia kwenye mtaro na
kuegama baadaye kuanguka upande wa kulia mwa gari. Katika ajali hiyo, watoto
wapatao 20 na walezi 5 waliweza kupata majeraha mbalimbali. Kati yao watoto 2
waliumia kichwani na kushonwa na walezi 4 walipumzishwa katika hospitali ya Mt.
Fransis kwa uchunguzi zaidi. Hadi tunaandika taarifa hii, watoto wote walio
pumzishwa wameruhusiwa na kati ya Walezi, ni mmoja tub ado yuko hospitali kwa
matobabu.
TUNAWAPA
POLE WOTE WALIOFIKWA NA AJALI HII NA KWA WALIOUMIA TUNAWAOMBEA WAPONE HARAKA.
Comments
Post a Comment